Pichani ni ushiriki wa Tanzania katika Mkutano wa Shirika la Msalaba Mwekundu Duniani ambao Rais wa Msalaba Mwekundu Tanzania ambapo Dr. Zainab Amir Gama na Mh. Balozi Modest Mero wanashiriki jijini Geneva Uswisi. Mkutano hio ulioanza tarehe 4 Desemba na utaisha leo tarehe 10 Disemba 2015.
Huu ni mkutano mkuu wa Msalaba Mwekundu na Hilari Nyekundu wa dunia ambao maudhui ya mkutano huu ni mjadala na maamuzi ya uongozi, amani, uhamiaji na unyanyasaji wa wanawake na watoto, mpango wa kupanua huduma za kibinadamu kufikiakaribu bilioni moja ifikapo mwaka 2030, umuhimu wa jumuiya za Msalaba Mwekundu na Hilari Nyekundu kuwa mdau mkuu wa serikali bila ya kwenda kinyume na misingi yao saba mwisho, ushiriki wa vijana na vile vile kuikaribisha nchi ya Tuvalu kuwa mwanachama wa 190.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...