Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alitoa agizo la kumtaka kila mtu kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya Uhuru tarehe 9 Disemba, 2015 kwa kushiriki zoezi la kufanya usafi wa mazingira. 
Katika Mkoa wa Dodoma, zoezi hilo litahusisha kazi za usafi wa makazi na maeneo ya shughuli mbalimbali, kufagia barabara za lami na vumbi, kufyeka nyasi kandokando mwa barabara na katika maeneo ya wazi na jamii, kuokota  takataka  (mifuko ya Rambo) na kuzibua mitaro ya maji ya mvua kama ipo katika  eneo husika kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana. 
Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa kupitia Ofisi zao ndio waratibu wa zoezi la usafi kwenye Wilaya husika. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma, ameainisha maeneo ambayo taasisi mbalimbali za Mkoa wa Dodoma zitayashughulikia kufanya usafi Mjini Dodoma (Orodha imeambatishwa). 
Kutokana na uhaba wa vifaa vya kufanyia Usafi. Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma anashauri taasisi mbalimbali zitakazohusika na zoezi la usafi wa mazingira, ziwe na vifaa vyake vya kufanyia usafi. 
Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma anasisitiza zoezi la usafi kwa taasisi, lizingatie maeneo yaliyotajwa kwenye  jedwali lililoambatishwa na Uongozi wa Serikali Mkoa wa Dodoma unamtaka kila mwananchi na taasisi zilizopo Dodoma kushiriki kikamilifu katika usafi huu.

Imetolewa na:
OFISI YA MKUU WA MKOA
DODOMA

Disemba 8, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...