Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Ally Simba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya Simu za Mkononi ya Vodacom imekidhi vigezo vya utoaji huduma kwa wateja huku makampuni matano yakipigwa adhabu ya sh.milioni 25 kutokana kulaghai wateja.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba amesema kuwa kampuni ambazo hazijaweza kuboresha huduma zao kuanzia leo ili kuweza wateja kupata huduma bila kuwepo kwa malalamiko.

Kampuni zilipigwa adhabu kutokana na kukiuka taratibu za kisheria za utoaji wa huduma za mawasiliano ni Tigo,Airtel,Halotel ,Zantel pamoja na Smart.

Simba amesema mitandao ya mawasiliano inaweka mazingira salama yatakyozuia utumaji wa ujumbe za kilaghai na matishio mengine ya kiusalama.

Amesema adhabu ya sh.milioni 25 kwa kampuni zilizokiuka sheria za utoaji wa huduma zinatakiwa kulipa kabla ya Januari 29.

Aidha TCRA imetaka kampuni ambazo zitashindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa hawataacha kuwachukulia hatua za kisheria kwa kampuni husika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...