Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa viongozi wa TPA (hawapo pichani), alipokuwa akizungumza nao juu ya masuala mbalimbali ya utekelezaji wa majukumu yao.
Maafisa wa Wizara na Watendaji wa Mamlaka ya Bandari wakimsikiliza kwa makini Mhe. Waziri Mbarawa alipokuwa akitoa maelekezo ya kazi katika ofisi za Meneja wa Bandari mkoa wa Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
BAADA ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufanya ziara katika Mamlaka ya Bandari Nchini (TPA) na kubaini uondoshwaji wa wa kontena 329 bila kulipiwa kodi ya zaidi ya sh.bilioni 12, Mawakala wa Forodha walifanya ukaguzi kuona kama kuna upotevu wa mapato na kubaini jumla ya kontena 11,884 na magari 2019 yalitolewa bila malipo.

Makontena hayo yalitolewa katika bandari kavu ni MOFED 61, DICD 491, JEFAG 1, 450, AZAM 295, PMM 779, AMI 4384, TRH 4,424 ambazo kodi yake ni zaidi ya sh.bilioni 47.

Magari 2019 yalitolewa bila kulipa kodi katika kampuni za TALL 309, CHICASA 65, FARION 18, SILVER 97, MASS 171, HESU 1359 na kuinyima nchi kodi yenye thamani ya zaidi ya tsh.bilioni moja (1).



Akizungumza na wafanyakazi wa Bandari jijini Dar es salaam leo, Waziri wa Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema wataendelea kuchukua hatua dhidi ya wale ambao wamehusika wakiwemo watumishi wanaoshiriki katika hujuma.

Wafanyakazi saba wa TPA wanashikiriwa na polisi kuhusiana na upotevu wa kontena hizo na kusababisha serikali kukosa mapato.

Waliotiwa mbaroni na jeshi la polisi baada ya kukamatwa leo ni John Elisante, Leticia Masaro, Christina Temu, Merina Chawala, Adnan Ally, Masoud Seleman na Benadeta Sangawe.

Wanaotafutwa kwa tuhuma za kusababisha upotevu wa kodi za serikali katika bandari ya Dar es Salaam ni Happygod Naftal, Nathan Edward, Aron Lusingu, Amani Kazumari, John Mushi, Valentine Sangawe, Benasweet Kamaina, Zainab Bwijo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...