Na
Kassim Nyaki.
Watumishi
wa Sekretarieti ya Ajira wameaswa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za
Utumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao, kwa kuwa kazi wanayoifanya ni
nyeti na inagusa maisha ya watu ambayo itahitaji watu waadilifu, wapenda haki
na mfano mwema kwa jamii.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angella
Kairuki amesema hayo leo wakati alipotembelea ofisi hiyo na kuzungumza na
Wajumbe wa Sekretarieti ya Ajira pamoja na Watumishi.
''Nataka
mzingatie uadilifu katika utendaji kazi wenu wa kila siku, maana nitawafatilia
kila hatua kwani ninataka Watumishi wa Umma waadilifu ili mwisho wa siku tuwe
na Utumishi wa Umma uliotukuka'' alisisitiza Kairuki.
Aliongeza
kuwa Watanzania wako wengi wenye sifa za kuajiriwa, ambao wanahitaji kupata
huduma bora na inayostahili kwa kuwa kila Mtumishi aliyeko katika Sekretarieti
ya Ajira aliajiriwa akijua Utumishi wa Umma una taratibu zake za kiutendaji, kwa
mujibu wa Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali na si vinginevyo.
Aidha, aliwataka Watumishi hao kutumia hazina kubwa ya Wajumbe wa Sekretarieti ya Ajira waliopo kwa kuwa anawafahamu, anajua uwezo wao katika kazi, kwakuwa walikuwa Watumishi waadilifu wa Umma na wa muda mrefu. Hivyo ushauri wao na maelekezo wanayotoa yakitumika vizuri yataisaidia sana Sekretarieti ya Ajira katika kutimiza malengo yake na kuwa chombo cha mfano wa kuigwa kiutendaji.
Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Wajumbe wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Bakari Mahiza alimpongeza Waziri huyo kwa kuchaguliwa kusimamia Wizara hii nyeti inayosimamia rasimaliwatu ambayo ni rasilimali muhimu sana katika taifa lolote na anaamini ujio wake utaongeza chachu katika utendaji wa Taasisi hiyo.
Kwa upande wake Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Exavier Daudi mbali na kueleza jinsi Mchakato wa Ajira unavyoendeshwa, mafanikio, changamoto na matarajio ya chombo hiko alimshukuru Waziri huyo kwa kuwatembelea na kumwahidi kufanyia kazi maelekezo na ushauri alioutoa.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Daudi Xavier (kulia) akieleza majukumu ya ofisi yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – UTUMISHI na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) alipoitembelea ofisi hiyo mapema leo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – UTUMISHI na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) (kulia) akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma alipoitembelea ofisi hiyo mapema leo.Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki akipata Maelezo ya juu wa upokeaji wa maombi ya kazi kwa njia ya Mtandao kutoka kwa Naibu Katibu wa Kitengo cha TEHAMA Mhandisi Samweli Tanguye.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...