Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kulia) akitoa maagizo ya kukamilika kwa mradi huo ifikapo february mwakani kwa Mkurugenzi Mwandamizi wa Miradi TANESCO Bw.Gregory Chegere (wa kwanza kushoto) alipofanya ziara yake leo katika mradi wa Tanzania Energy Development Access Program (TEDAP) eneo la Mbagala Rangi Tatu,jijini Dar es Salaam,Mradi huo utasaidia kusambaza umeme wenye nguvu ya kutosha na unaotarajia kunufaisha zaidi ya wananchi elfu kumi wa eneo hilo,watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Paul Masanja.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (kushoto) akitoa maagizo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya SAE Power Lines Bw.Tahir Mehmood (wa kulia) anayejenga mradi wa TEDAP eneo la Kurasini jijini Dar es salaam kuhakikisha mpaka mwanzoni mwa mwakani awe amshafunga Transifoma katika eneo hilo la mradi ni baada ya kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wake katika mradi huo.
Mhandisi Mkuu wa Miradi TANESCO Bw. Frank Mashalo (wa kwanza kulia) akimweleza Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa pili kushoto)kuhusu maendeleo ya mradi TEDAP uliyopo maeneo ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam na (wa kwanza kushoto) ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Paul Masanja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...