Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi akizungumza na wakuu Idara katika wizara ya Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi alipokutana nao leo alipokaribishwa kwa mara ya kwanza katika wizara hiyo, tangu achaguliwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa wizara, na kuwaagiza wakuu wa idara katika wizara hiyo kutoa taaarifa za idara zao ifikapo jumatatu ya wiki ijayo.
Naibu Waziri wa Wizara Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akizungumza na wakuu wa Idara wa wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam, akizungumzia kuhusiana na wawekezaji ambao watakua hawajaendeleza ardhi ambayo walichukua kwa aajili ya uwekezaji na ardhi hiyo kurudishwa kwa wananchi. Kutoka Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara ya Ardhi Nymba na Maendeleo ya Makazi, Alphayo Midata, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Ardhi, Nymba na Maendeleo ya Makazi, Selassie Mayunga.
Baadhi ya waandishi wa habari pamoja na wakuu wa Idara za wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...