Shirika la ndege la bei nafuu lapanua
wigo wa safari zake barani Afrika na kufungua safari ya kimataifa ya moja kwa
moja kutoka Nairobi kwenda Dar es Salaam na Kilimanjaro.
Kampuni ya Fastjet imetangaza safari yake mpya ya kimataifa
ya kutoka Dar es Salaam kwenda Nairobi, Kenya kuwa itaanza rasmi mnamo tarehe
11 Januari 2016.
Fastjet imepewa ruhusa na serikali ya
Kenya kufanya safari zake nchini humo kufuatia makubaliano ya pamoja na mashirika
yanayotoa huduma za usafiri wa anga kati ya nchi hizi mbili za Tanzania na
Kenya, kama ilivyopitishwa na serikali ya Tanzania.
Vilevile Fastjet imetangaza kuwa
inatarajia kuzindua safari zake za anga kati ya Zanzibar na Nairobi na pia kati
ya Dar es Salaam na Mombasa ambapo uzinduzi huo utafanyika mapema mwaka huu
2016.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...