TAARIFA KWA UMMA

Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali anakusudia kuyachukulia hatua Mashirika yanayoendesha shughuli zao kinyume cha Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005. 

Mashirika hayo ni yale ambayo hayajawasilisha taarifa za mwaka kwa kipindi cha miaka miwili pasipo kutoa sababu za msingi, kulipa ada ya mwaka au kuendesha shughuli za NGOs bila kusajiliwa chini ya Sheria ya NGOs.
Kwa taarifa hii, Mashirika husika yanatakiwa yawe yamerekebisha dosari tajwa ndani ya siku thelathini (30) kuanzia tarehe ya tangazo hili. Baada ya kipindi hicho, Msajili wa NGOs atayafutia usajili Mashirika ambayo yatakuwa hayajawasilisha taarifa na kuyachukulia hatua stahiki Mashirika yanayoendesha shughuli za NGOs bila ya usajili chini ya Sheria husika.
Malipo yote ya ada yafanyike kupitia Benki ya NMB, NGO Account Na. 20110014074 na stakabadhi halali ya malipo itumwe kwa Msajili wa NGOs.

                                                      Imetolewa na:

M.S. Katemba
MSAJILI WA NGOs
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, 
JINSIA, WAZEE NA WATOTO
 06 Januari, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...