Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe. Hamad Masauni akiwa katika ziara yake kutembelea mradi wa kisima cha maji kaburukikombe migimbani Zanzibar.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Hamad Yussuf Masauni akizungumza na Wananchi wa Jimbo hilo wakati wa ziara yake katika mradi wa maji kaburi kikombe migombani Zanzibar Mradi huo unasimamiwa na Jumuiya ya TAYI Tanzania Youth Icon kulia aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Rahaleo na kwa sasa anagombea Jimbo la Kikwajuni Zanzibar Mhe Nassor Salim Jazira.
Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni akiangalia mradi wa kisima kipya kinachosimamiwa na TAYI kinachochimbwa katika eneo la Kaburi Kikombe Zanzibarb hicho kitakuwa kisima cha Pili kuchimbwa na TAYI kwa Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni kikiwa na urefu wa mita 42 kinachotarajiwa kukamilika kwake kutumia shilingi milioni 20 hadi kukamilika kwake.
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya TAYI Abdalla Ahmeid akitowa maelezo ya mradi huo wa Pili wa Uchimbaji wa Kisima cha Maji kwa ajili ya Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni na jirani zake kikiwa katika hatu ya mwisho ya uchimbaji wake. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...