WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro na kuzungumzia fursa mbalimbali za uwekezaji nchini hususan katika sekta ya Nishati.

Muro alimtembelea Waziri Muhongo na kueleza nia ya Kampuni yake kuwekeza kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirishia mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza na vilevile uwekezaji kwenye mradi wa ujenzi wa nguzo za umeme za zege. 
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo pichani) ambaye alimtembelea Waziri huyo kuzungumzia fursa za uwekezaji kwenye sekta ya nishati nchini. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu- Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza jambo wakati wa kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe na wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu- Nishati, Dkt. Mhandisi, Juliana Pallangyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...