LIGI Daraja la kwanza inaendelea kesho kwa michezo miwili huku timu ya Friends Rangers (pichani) ya Dar es salaam ikishuka kwenye Uwanja wa mabatini Mlandizi kuvaana na timu ya KMC.

Ofisa Habari wa klabu ya Friends Rangers, Asha Kigundula, alisema kuwa wanatambua ugumu wa mechi hiyo lakini lengo lao ni kushinda na kupata pointi tatu.
Kigundula alisema anatambua kama wapinzani wao wamejipanga kushinda, lakini nao wapo kwa lengo la kufanya vizuri na kuondoka na pointi tatu.
Alisema wao hawajataka tamaa wana amini bado wana nafasi ya kupigania kupanda daraja na kucheza ligi kuu msimu ujao.
"Mechi ngumu sana lakini tumejipanga kushinda mchezo wetu huu, tunatambua uzuri wa KMC lakini nasi tuko vizuri kama tulivyowatoa kwenye michuano ya FA Cup.
Alisema kuwa wapo katika nafasi nzuri ya kupigana na kufanikiwa kuvuka vizingiti wanavyowekewa na baadhi ya wadau wengi.
Wakati huo huo mechi nyingine ya ligi hiyo itakuwa kati ya Africa Lyon dhidi ya Kiluvya United mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Karume.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...