Shule ya Sekondari ya St. Jude ya jijini Arusha kwa namna ya pekee wameelewa azma na malengo ya Shule Direct. Hawakuwahi kuwaambia Shule Direct kwa maneno lakini takwimu zinaelezea ukweli huu.
Ni shule inayoongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wanaojifunza kupitia tovuti ya Shule Direct kuliko Shule nyingine yoyote; na kufuatiwa na Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Azania na ya tatu ni Shule ya Sekondari ya Kibasila.
Wanafunzi wa shule hizi wametumia muda mwingi zaidi kujifunza kupitia Shule Direct kuliko watumiaji wengine.
Shule hizi ni mfano wa kuigwa kwa sababu maarifa hayana mipaka, kadri tunavyojenga hulka ya kutafuta na kujifunza kwa kutumia fursa mbali mbali, hivyo ndivyo wanafunzi watakavyokuwa hata pale watakapokuwa wamemaliza shule.
Kwa namna ya pekee, Shule Direct wanawapongeza na kuwasifu shule ya St. Jude kwa sababu wamekuwa mfano wa kuigwa.
Shule Direct ni
taasisi inayoboresha fursa za mwanafunzi kuweza kusoma, kufanya mazoezi na
kujadiliana katika masomo mbalimbali na wanafunzi wenzake pamoja na walimu kwa kutumia
Teknolojia.
Elimu bora ni haki ya kila mtoto na kila mwanafunzi. Ukuaji wa
Teknolojia Tanzania na barani Afrika kwa ujumla unapaswa kuwa nyenzo ya
kuboresha upatikanaji wa maarifa na elimu ambapo kuna changamoto nyingi zinazowazuia
wanafunzi kuipata.
Shule Direct inaamini kwamba elimu inapaswa kupatikana saa
yoyote na mahali popote kwa sababu elimu ni chachu ya kubaini uwezo na vipaji
vilivyomo ndani ya mtu.
Wanafunzi walioongoza kujifunza kupitia Shule Direct kutoka Shule ya St. Jude, (kwa kutumia majina yao ya kujisajili, wala si majina yao kwa kweli), ni iBOY, Brightstar, Nasmar, Mkavi, Chrisspros, Mathew.bob, Muller, Amaur, Shabbb, Jariss.j.jr. Tunawazawadia wanafunzi hawa “digital coins” za Shule Direct zitakazowawezesha kununua vitabu na vifaa mbalimbali kupitia hapo hapo kwenye tovuti.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...