Na Raymond Mushumbusi MAELEZO

Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA) imesema itaendelea kupambana na wale wote watakaogundulika kwa wizi wa kazi za sanaa.

Agizo hilo limetolewa na Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Alphayo Kidata alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari na kueleza kuwa wapo katika operesheni ya kukamata wezi wa kazi za sanaa .

"Ipo  kamati ambayo inajumuisha wadau kama Bodi ya Filamu, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na COSOTA ikishirikiana na Jeshi la Polisi katika  kupambana na wizi wa kazi za wasanii unaokidhiri siku hadi siku' `Alisema Kaimu Kamishna Kidata.


Serikali ipo makini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania katika kukusanya mapato hasa kuongeza maeneo ya kukusanya mapato ikiwemo eneo la kazi za sanaa hivyo  Serikali haitakubali kuona inakosa mapato hayo na yoyote anayejua mtu au kikundi cha watu kinachofanya wizi wa kazi za sanaa atoe taarifa ofisi za TRA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...