Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa
nchini, Lu Youqin akizungumza katika kikao na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mhe. Charles Kitwanga (wa pili upande wa kushoto). Katika kikao hicho kilichofanyika Wizara
hapo, viongozi hawa walijadili masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano wa
Serikali ya China na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe.
Charles Kitwanga (wa kwanza upande wa kulia), akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya
Watu wa China nchini Tanzania, Lu Youqing (wapili upande wa kushoto) wakati wa mazungumzo
yaliyohusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati Serikali ya China na Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi jijini Dar es Salaam..
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles
Kitwanga (kulia), akizungumza na ujumbe wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, ulioongozwa na Balozi LuYouqing,
(hawapo pichani), katika mkutano uliojumuisha pande hizo mbili kuzungumzia
masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Serikali ya Watu wa China na Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini
Tanzania, Lu Youqing , akisaini kitabu cha wageni mara baadaya kuwasili katika
Ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia), ofisini kwake
alipowasili Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa ziara fupi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles
Kitwanga (wa nne kutoka kulia), akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka
Ubalozi wa China nchini Tanzania, ulioongozwa na Balozi Lu Youqing (watatu kutoka
kulia). Ujumbe huo ulitembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kujadili
masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa
China na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.(PICHA
NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI – WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...