Katika ziara hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Charles Kitwanga amelisisitizia Jeshi hilo kuimarisha ukaguzi katika majengo marefu na mafupi ikiwemo vyombo vya usafiri na usafirishaji. Pia Mhe. Waziri amesisitiza kusimamia sheria ya maokozi inayowataka wananchi kupisha magari ya Zimamoto pamoja na gari la wagonjwa pindi yanapokuwa katika dharura. 
“Hivi hamjui hata msafara wa Rais unalazimika kupisha gari la Zimamoto au wagonjwa? Iweje leo wananchi wasipishe magari hayo? Simamieni sheria hii” Alisisitiza Mhe. Waziri. 
Aidha Mhe. Waziri aliahidi kushughulikia changamoto zote zinazolikabili Jeshi hilo changamoto hizo ni ukosefu wa vifaa, ufinyu wa bajeti pamoja na idadi ndogo ya Askari.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Charles Kitwanga akipewa maelezo kutoka kwa Kamishna Jenerali Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Eng; Pius Nyambacha jinsi ya upokeaji taarifa za matukio katika chumba cha mawasiliano tarehe 08/01/2016. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Charles Kitwanga atembelea Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na kukagua mitambo ya kuzimia moto pamoja na maokozi, kulia ni Eng; Pius Nyambacha Kamishna Jenerali Jeshi la Zimamoto na Uokoaji tarehe 08/01/2016. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Charles Kitwanga akipewa maelezo kutoka kwa Sajini Christopher Marwa jinsi ya kutumia vifaa vya maokozi katika gari maalumu la maokozi alipofanya ziara katika Jeshi hilo tarehe 08/01/2016. (Picha na Kitengo cha Habari Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sijui watakua wamekumbuka kusema mzee wajua tatizo letu kubwa maji, hua yanatuishia kabla hata hatujafika eneo la tukio hali inayopelekea wananchi kuzima moto kwa kutumia ndoo na sisi kupigwa mawe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...