Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Mbogo Futakamba akitoa zawadi kwa mfanyakazi bora wa mwaka 2015 toka DAWASCO wakati alipotembelea Shirika hilo mapema wiki hii. Pamoja na mambo mengine alielekeza shirika juu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Serikali ya kuunganisha Wateja Milioni Moja ifikapo June 2016. Picha na Everlasting Lyaro- DAWASCO.

WIZARA ya maji na umwagiliaji, imesema inaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mipango ya usambazaji wa huduma za maji, inayofanywa na shirika la majisafi na majitaka jijini Dar es Salaam (DAWASCO) na kutoa rai kwa watumishi wa shirika hilo kushirikiana ili kufikia malengo ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hayo yalisemwa jana na katibu mkuu wa wizara hiyo mhandisi Mbogo Futakamba, alipokuwa akiwahutubia wafanyakazi wa DAWASCO, katika makao makuu ya shirika hilo jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Futakamba, alisema kasi ya utoaji wa huduma bora za maji kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam, imepunguza malalamiko mengi ya wananchi, na kwamba serikali imeanza kupata matumaini makubwa na kujenga imani kwa shirika hilo kwa kufanikisha malengo makuu ya usambazaji wa huduma hiyo kwa wananchi.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...