Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa za Kuwekeza cha benki hiyo, Andrew Massawe (kushoto), akizungumza kuhusu faida mbalimbali za mteja wa benki hiyo atakayeshiriki kampeni ya malengo ya NBC. Kulia ni Mkuu wa Huduma za Rejareja za Kibenki wa benki hiyo, Mussa Jallow.
Mkuu wa Huduma za Rejareja za Kibenki wa benki ya NBC, Mussa Jallow (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi kampeni ya Malengo ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja Masoko wa NBC, Alina Maria Kimaryo na kulia ni Meneja wa kampeni hiyo, Mtenya Cheya.
Kampeni ya malengo itadumu kwa muda wa miezi mitatu kutoka Februari 4 mpaka Aprili 30 2016. Katika kipindi hicho cha miezi mitatu ya kampeni,wateja wanaoweka fedha watafaidika na kiwango cha kuvutia cha riba na kuwa katika nafasi kubwa ya kushinda gari mpya aina ya Toyota Land Cruiser Prado kama linavooeneka pichani.
Mkuu wa Huduma za Rejareja za Kibenki wa benki ya NBC, Mussa Jallow (kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa za Kuwekeza cha benki hiyo, Andrew Massawe.
mmmh hizi picha zilipigwa kwa simu nini? tena mchina. kitengo cha PR nunueni camera ya kisasa mpost picha zinazoeleweka acheni hizo.
ReplyDelete