Vyuo vya elimu ya juu nchini vyatakiwa kuzingatia zaidi ubora wa elimu vinayotoa ili kuzalisha wasomi na wataalamu wenye tija kwa taifa.https://youtu.be/xow5pIxeW4w
Mawasiliano ya barabara kati ya mkoa wa Dodoma na Morogoro yako hatarini kukatika kufuatia mafuriko makubwa yaliyotokea katika barabara kuu katika eneo la Kibaigwa. https://youtu.be/aypFBv6ZM0M
Serikali yakamilisha ukaguzi wa mgodi wa madini wa Tanzania One ulioko Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara kufuatia agizo la kamati za ulinzi na usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara baada ya wafanyakazi wa mgodi huo hapo awali, kudai uwepo wa dalili za baadhi ya sehemu za mgodi huo kutaka kudidimia hivyo kuhatarisha maisha yao.https://youtu.be/uim_W8zduyw
Katika kuadhimisha siku ya sheria nchini mahakama mkoani Shinyanga yaahidi kushughulikia kwa ukamilifu yeyote atakayepatikana na hatia ya kujihusisha na vitendo viovu ikiwemo mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.https://youtu.be/f0Dhl-Yqub8
Tume ya ushindani yaendesha operesheni ya kukamata bidhaa bandia katika maeneo ya Kariakoo baada ya kupokea malalamiko juu ya uwepo wa bidhaa hizo kutoka kwa mawakala halali wanaoingiza bidhaa hapa nchini.https://youtu.be/q4n9QRhEorU
Rais John Magufuli aagiza kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi haraka ili kupambana na mafisadi wa mali za umma; https://youtu.be/EQuSFvAqVV4
Msajili mkuu wa vyama vya siasa nchini, avitaka vyama vya siasa, NEC na ZEC kutumia busara katika mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani Zanzibar;https://youtu.be/9DgyNCEjs9Q
Fahamu alichokisema waziri wa mamabo ya nje, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga kuhusu wanafunzi wa kitanzania kushambulia nchini India;https://youtu.be/uVx1npk-cjw
Inaelezwa jiji la Mwanza bado linakabiliwa na changamoto ya kupambana na ugonjwa wa kipindupindu unaozidi kuenea kwa kasi jiji humo;https://youtu.be/ODfaFl7gO68
Inaelezwa kuwa shule takribani tano katika kata ya Bunju jijini Dar es Salaam zinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa vyoo; https://youtu.be/D-_muVTyUxs
Madiwani wilayani Geita washauriwa kuwa mfano katika kubuni miradi ikayowasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi; https://youtu.be/zdyfmDByYHE
Timu ya Tanzania Prisons ya jijini Mbeya yaahidi kutokupoteza mchezo wowote wa ligi kuu katika uwanja wake wa nyumbani; https://youtu.be/kQzxSTIV-ic
Mgombea wa Urais wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA, Gianni azidi kung’ara mara baada ya nchi ya Urusi kutanganza kumuunga mkono;https://youtu.be/L0LE21CaQbc
Wadau wa sheria nchini washauriwa kushirikiana vizuri na mahakama ili kuharakisha utoaji wa haki kwa wakati; https://youtu.be/rYtBjELDYDE
Wizara ya maliasili na utalii yasema bado inaeendelea na msako mkali kuwasaka majangili waliohusika na kutungua helikopta katika mbunga ya wanyama ya Serengeti; https://youtu.be/zb6Dg0htV7s
Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Abdulrahman Kinana awasili mkoani Singida kushiriki shughuli mbalimbali za kimaendeleo kama sehemu ya maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama hicho; https://youtu.be/3Vw46tMfnxs
Jumuiya ya wanawake wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Mbulu mkoani Manyara waadhimisha sherehe ya kuzaliwa kwa chama hicho kwa kumjengea nyumba mjane; https://youtu.be/IUsYPeQzRXo
Waziri mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuzindua mwongozo wenye lengo la kumwezesha mwananchi kujikwamua kiuchumi;https://youtu.be/qWqzGXf1SjM
Wachezaji wa soka nchini washauriwa kucheza kwa nidhamu na ushirikiano ili kufukia malengo yao; https://youtu.be/TIPF0w1O2p0
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...