Msama alisema albamu hiyo ni moto wa kuotea mbali, hivyo wakazi wa mikao ya Kanda ya Ziwa kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha hilo ambalo litashi8rikisha waimbajki mbalimbali wa Tanzania.Msama alizitaja nyimbo zilizoko kwenye albamu hiyo ni pamoja na Ipo siku, Acha waambiane, Haohao, Nisamehe, Pendo langu, Ndiwe Mungu, Moyo tulia na Surprise.Aidha Msama alitumia fursa hiyo kueleza kwamba viingilio katika tamashja hilo ni shilingi 5000 kwa wakubwa na watoto shilingi 2000.
"Tamasha la Pasaka ni sehemu ya kusaidia wenye uhitaji maalum ambao ni pamoja na walemavu, yatima na wajane ambao wanahitaji msaada kutoka kwa wadau kama kampuni ya Msama Promotions," alisema Msama.
Msama aliwataja waimbaji waliothibitisha kushiriki katika tamasha hilo ni pamoja na Rose Muhando, Bonny Mwaitege, Upendo Nkone, Jesca BM Honore, Jennifer Mgendi, Sifael Mwabuka, Joshua Mlelwa, Martha Baraka, Christopher Mwahangila, Anastazia Mukabwa, Kwaya ya AIC Makongoro, Kwaya ya Wakorintho wapili, Faustine Munishi, Solomon Mukubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...