Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akijitambulisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kabla ya Kamati hiyo kuipokea taarifa ya Wizara hiyo katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo baada ya kuundwa na Bunge hivi karibuni. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu anayefuatia ni Makamu wake, Kanali Masoud Khamis. Kulia kwa Masauni ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Mohamed Rajabu akizungumza jambo na Wajumbe wa Kamati yake pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika kikao chao kwanza tangu Kamati hiyo iundwe na Bunge hivi karibuni. Wapili kulia mstari wa mbele ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni, na kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Kanali Masoud Khamis. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akitoa taarifa ya Wizara katika kikao cha kwanza cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kikao hicho kilichohudhuriwa na Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Maafisa wa Wizara, kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...