Na  Bashir  Yakub .

Masuala  yanayohusu  ardhi  ni  masuala  nyeti  sana.  Unyeti  wa  masuala  haya  unatokana  na  ukweli  kuwa  maisha yote  yamejengwa juu  ya  ardhi. Hakuna kilichowahi  kufanywa, kinachofanywa  na  kitakachofanywa nje  ya  ardhi. Iwe  kutembea,  kuendesha  kipando, kula, kulala, maendelezo  yoyote  ya  teknolojia, ujenzi,  maji  safi  na  salama, kupata  chakula, hata  unaporuka  hewani  iwe  kwa  ndege  au  kifaa  kinginecho  huwezi  kusema  sijatumia  ardhi kwakuwa hata  mruko  wenyewe(take off) huanza  na  ardhi. 

Lakini pia hata  uruke  na  ukae  huko  miaka  200  bado  utatakiwa  kurejea ardhini.  Ardhi  ni  kila  kitu kwa  maana  ya  kila kitu.  Kupitia  msingi  huu  tunapata    umuhimu  mkubwa  wa  kueleza  kila  lililo  la  msingi  kuhusiana na masuala  ya ardhi  hususan umiliki wake. 

Kupitia  makala  hizi   yalishaelezwa  mengi  kuhusu  namna  ya  kununua  ardhi,  namna  ya  kuepuka  migogoro  wakati  wa  ununuzi,  namna  ya  kubadilisha  hati  na  mengine . Fursa   ya  leo  itaeleza  umuhimu  na  faida  za  kuwa  na  hati.

1.NINI  MAANA  YA  HATIMILIKI .
Hati  miliki  ya  ardhi  hujulikana  pia  kama  “Title  Deed”.  Hatimiliki  ya  ardhi  ni  nyaraka  maalum  inayotolewa   na  wizara  ya  ardhi ikionesha  mwenye  haki  ya  umiliki wa  ardhi, eneo  na  kiasi  anachomiliki  huku  ikiainisha  wajibu  na  haki  alizonazo  mmiliki  huyo. 

Wajibu  katika  hatimiliki  ni  yale  unayotakiwa  kutekeleza  kwa  mfano  malipo    ya  kila  mwaka,  matumizi  yaliyopangwa, na  kila  sharti  analotakiwa  kutekeleza  mmiliki.

Haki  katika  hatimiliki  ni  yale yote  anayostahili kupata  mmiliki  wa  ardhi  husika  ikiwemo  taarifa ( notice) rasmi  panapo  mabadiliko yoyote  katika  matumizi  na  umiliki, haki  ya  fidia,  na  haki  ya  kuwa   huru  katika  matumizi  halali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...