Na  Bashir  Yakub.

Mara  kadhaa  tumeeleza  namna  ya  kusajili  kampuni. Yumkini  tulipoeleza  hivyo  tulirejea usajili  wa  kampuni  zilizo  Tanzania.  Tulieleza  faida  za  kufanya  biashara  chini  ya  kampuni  na  tukaeleza  namna  ya  kisheria  ya  kusajili  kampuni  mwanzo  mpaka  mwisho  unapopata  cheti  cha  kuzaliwa  kwa  kampuni( certificate  of  incorporation). Hatujawahi  kueleza  usajili  wa  kampuni  ambayo  imeanzishwa  nje  ya  Tanzania inayohitaji  kufanya  biashara  Tanzania.

1.KAMPUNI  ILIYOSAJILIWA  NJE  YA  TANZANIA.

Tunaposema  kampuni  kusajiliwa  nje  ya  Tanzania  tunamaanisha  kampuni   imeanzishwa  nje  ya  Tanzania    na  cheti  chake  cha  usajili  imekipata  huko  nje  ya  Tanzania  na  hivyo  inatambulika  kama  kampuni  ya  huko  ilikosajiliwa.  Kampuni  ya  namna  hii  inaweza  kuamua  kuja  Tanzania  kufanya  biashara  bila  kuhitaji  kuanzisha  kampuni  nyingine  mpya  isipokuwa   kuendeleza  ileile  na   kupafanya Tanzania kama  tawi  au  si  tawi   lakini sehemu  kuu  ya  biashara.

2.  WATANZANIA  WALIO  NJE  YA  NCHI  KUMILIKI  MAKAMPUNI  HAYA.

Baadhi  ya  Watanzania  walio  nje  ya  nchi  wamewahi  kuuliza  swali  hili  wakitaka  kujua  utaratibu  wa  kufuata  ili  kuifanya  kampuni  iliyoanzishwa nje  ya Tanzania kuweza kufanya  kazi  zake  Tanzania. 
Kwa  waliouliza  swali  hili  watapata  majawabu  lakini  pia itafahamika  kwa  wengine  kuwa  unaweza  kuunda  kampuni  hukohuko  uliko  ikafanya  kazi  huko  lakini  pia  Tanzania  ambako  ni  nyumbani  kukawa  na  tawi  la  biashara  . 

Lakini  pia  wapo  watu  ambao  huulizwa  swali  hili na  rafiki  zao  wa  kigeni  kuhusu  kuingiza  kampuni  Tanzania   kwa  ajili  ya  biashara.  Hawa  nao  sasa  watakuwa  na majawabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...