MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali.

Uzinduzi huo uliofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam leo na kuhudhuliwa na watu mbalimbali wakiwepo wakenya, waganda na watanzania na watu kutoka bara la Ulaya na Asia.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu amesema kuwa wanawake ni watendaji wazuri na wanamaamuzi mazuri katika uongozi na uendelezaji wa makamuni pamoja na Tasisi mbalimbali.

Mpango huo uliozinduliwa leo umefanywa wanachana chama cha  waajili Tanzania ambao unalenga kuwajengea uwezo wanawake ili kuongeza ufanisi katika biashara zao na kujenga mtandao ambao utaongeza juhudi na maarifa kwa wanawake.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa kuzindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam leo.
Makamu Mwenyekiti wa kampuni ya ATE, Zuhura Muro akizungumza na wanawake kutoka kutoka makampuni mbalimbali leo wakati Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua mpango malumu wa kuwafundisha wanawake ili waweze kuwa na uwezo wa kuleta mawazo yenye kuinua kampuni au taasisi mbalimbali kuwa kubwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja baada ya kuzindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam leo.

Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...