Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani akionesha Kifaa cha ‘Lead Board’ kwa viongozi wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma (hawapo pichani) hivi karibuni. Dk Kalemani alikutana na viongozi hao wakati wa ziara yake wilayani humo kukagua miradi ya umeme inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba.
Fundi Umeme, akifunga umeme wa REA kama alivyokutwa na Msafara wa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani, eneo la Buselesele mkoani Geita hivi karibuni. Naibu Waziri alikuwa katika ziara ya kazi kukagua miradi ya umeme vijijini.
Na Veronica Simba - Kakonko
Serikali imesema, wananchi wa kipato cha chini, hususan wa vijijini, wenye nyumba zenye kuanzia Chumba kimoja hadi Vinne, wataunganishiwa umeme pasipo kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwenye nyumba zao.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani, aliyasema hayo hivi karibuni Wilayani Kakonko, mkoani Kigoma, akiwa katika ziara ya kazi mkoani humo, kukagua miradi inayotekelezwa chini ya wizara yake, hususan ya umeme vijijini, kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
Dk Kalemani alisema, badala ya kutandaza nyaya za umeme katika nyumba zao, wananchi hao watafungiwa kifaa maalum kijulikanacho kitaalam kama ‘Lead Board’, kitakachowawezesha kutumia umeme kama kawaida.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...