Na Teresia Mhagama, Mtera

Imeelezwa kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kutafuta fedha  kwa   ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ambayo wananchi  wameamua kuiendeleza  ikiwemo miradi ya uzalishaji umeme kwa kutumia vyanzo mbalimbali kama maji,upepo, jua, nishati  jadidifu, makaa ya mawe na mawimbi ya bahari. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo wakati wa kikao chake na wazalishaji wa umeme wa maji na wale wanaotaka kuzalisha umeme huo chini ya megawati 20 kilichofanyika katika Kituo cha Kuzalishia Umeme cha Mtera. 

“Serikali lazima iwe Msemaji wa wawekezaji hawa ili kuhakikisha wanapata fedha na teknolojia za kuendesha miradi yao na hii itapelekea Taifa kuwa na nishati ya kutosha kwani wawekezaji hawa sasa watakuwa na uwezo wa  kuzalisha umeme,” alisema Profesa Muhongo. 

Ili kufanikisha suala, Profesa Muhongo  aliwataka wadau hao wanaotaka kuzalisha umeme wa maji chini ya megawati 20 kuhakikisha kuwa wanaandika na kuwasilisha wizarani mapendekezo yanayochanganua  miradi  wanayotaka  kuanzisha kabla ya mwisho wa mwezi huu ili litengenezwe kalabrasha moja litakalotumika katika kuombea fedha kwa wafadhili mbalimbali na Taasisi za Kifedha. 

“Ifikapo tarehe 28 mwezi huu mchanganuo wa mapendekezo yenu yawe yamemfikia Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Nishati ili serikali iangalie namna ya kutafuta fedha zitakazowawezehsa  kuendeleza miradi yenu ya  umeme badala ya  mtu mmoja mmoja kuanza kuzunguka na maombi yake binafsi  ya kutafuta fedha kutoka Taasisi mbalimbali jambo linalochelewesha upatikanaji wa fedha hizo, “ alisema Profesa Muhongo. 

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...