Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) liliandaa semina ya waandishi wa Mkoa wa Mtwara, Semina hiyo ililenga kuwajengea uwezo waandishi hao kuielewa sekta ya mafuta na gesi asilia mchini.
Akifungua semina hiyo kwaniaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Meneja wa Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu alisema semina hiyo anaamini itawajengea uwezo waandishi hao hasa wanapo toa taarifa za mafuta na gesi asilia kwa wananchi.
Watoa mada katika semina hiyo kutoka TPDC walitoa mada zilizo gusa shughuli nzima za Shirika kuanzia utafiti wa gesi asilia na mafuta hadi matumizi ya rasilimali hizo.
Kwa upande wao waandishi wa habari walioshiriki semina hiyo wameipongeza TPDC kwa jitihada hizo za kutoa mafunzo kwao, zaidi waandishi hao wametaka mafunzo hayo yawe endelevu kwao.
 Meneja wa Mawasiliano kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Marie Msellemu akifungua semina ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Mtwara, semina hiyo ilifanyika Manispaa ya Mtwara Mikidani huku ikilenga kuwajengea uwezo waandishi hao katika kuilewa tasnia ya mafuta na gesi asilia nchini.
Meneja wa Biashara ya Gesi kutoka TPDC Emmanuel Gilbert (kulia) akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Mtwara.
 Waandishi wa habari kutoa Mkoa wa Mtwara walioshiriki semina hiyo.
Katibu wa Klabu ya waandishi wa habari Mtwara Bw. Brayson Mshana akichangia jambo katika semina hiyo.
 Wawezeshaji wa semina kutoka TPDC wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari kutoka Mkoa wa Mtwara.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...