Baadhi ya walimu wa shule za msingi na sekondari wa Halmashauri ya Itigi,wilayani Manyoni,Mkoani Singida wakiwa katika ukumbi wa mkutano wa shule ya msingi Itigireli wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa CWT.
 Katibu wa idara ya Utumishi wa walimu(TSD) Mkoa wa Singida,Bwana Ole Saitabau(anayeandika mahudhurio katika kitabu) na kulia kwake ni kaimu afisa elimu Mkoa wa Singida.
 Naibu katibu Mkuu wa CWT,Bwana Eliezer Oluoch akizungumza na walimu wa shule za msingi na sekondari wa Halmashauri ya Itigi.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)
 Ni Majengo ya ofisi za muda za Halmashauri ya Itigi


Na Jumbe Ismailly,Itigi        
WILAYA ya Manyoni,Mkoani Singida inaongoza Mkoani hapa kwa kushindwa kushughulikia kero zinazowakabili walimu wa wilaya hiyo,na hivyo kusababisha malalamiko yasiyofanyiwakazi kuongezeka siku hadi siku.
Hayo yamebainishwa na walimu wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Itigi na Halmashauri ya wilaya ya Manyoni waliohudhuria katika kikao kilichoandaliwa rasmi kuonana na Naibu katibu mkuu wa cwt alikuwa na ziara ya siku moja wilayani Manyoni.
Wakizungumza kwa hasira kali kutokana na matatizo yao wanayowasilisha kwa afisa utumishi wa wilaya ya Manyoni na kwa katibu wa idara ya utumishi (TSD) wilaya hiyo,walimu hao wameweka wazi kwamba imekuwa ni kawaida kwao kunyanyaswa na watendaji hao wawili kila wanapokwenda kupeleka matatizo yao.
Mmoja wa walimu hao ambaye pia ni mratibu elimu wa kata ya Tambukareli,katika Halmashauri ya Itigi,Edsoni Nkinga alisema kwamba wamefurahia kusikia kati ya Halmashauri zenye matatizo Manyoni inaongoza kwa kushindwa kusikiliza na kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya walimu wa wilaya hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...