Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Chacha (katikati)akizungumza na wananchi juu ya kuwashukuru sana wapiga kura wake wa kata ya Vijibweni kwa kumchagua kuwa Diwani pamoja uongozi wa chama chake kwa kukubali kumpa nafasi ya kugombea kiti hicho, Jiji la Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Bw.Freeman Mbowe akizungumza na wananchi baada ya ushindi wa kiti hicho cha meya wa Jiji la Dar es Salaam.
Wafuasi wa chadema wakingombania bendera mara baada ya uchaguzi huo Jijini Dar es Salaam leo.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Chacha akisindikizwa na wananchi wa kuelekea Makao Mkuu ya Chama hicho,leo Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wafuasi wa Chadema waliojitokeza katika uchaguzi huo, leo Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)
KAIMU Mkurugenzi
Jiji la Dar es Salaam Bi. Sara
Yohana amemtanganza Isaya Chacha Diwani wa
Kata ya Vijibweni (CHADEMA)
kutoka Wilaya ya Temeke kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam mara baada ya
Uchaguzi.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema hayo mara baada ya uchaguzi
uliyofanyika leo jijini Dar es Salaam
ambapo mshindi alipata kwa kura 84 dhidi ya mgombea mweza kupitia chama cha CCM
Bw.Yenga Yusuph ambaye alipata kura 67,na katika uchaguzi huo kura 7
ziliharibika.
“Tunawashuruku wapiga
kura wote mlioshiriki zoezi hili la upigaji kura kwa utulivu bila vurugu na
kuweza kulifanikisha mpaka kumpata Meya wa Jiji hili”,alisema Bi Yohana.
Kwa upande wa mshindi wa Kiti cha Meya wa Jiji Mhe. Chacha alisema anawashukuru sana
wapiga kura wake wa kata ya Vijibweni kwa kumchagua kuwa Diwani pamoja uongozi
wa chama chake kwa kukubali kumpa nafasi ya kugombea kiti hicho.
“Nimejipanga kuleta maendeleo katika sekta ya elimu pamoja na
kupambana na kero ya foleni katika jiji pia hakikisha wananchi wote maskini
wanafaidika na mapato ya jiji hili
katika kuendeleza miundombinu mbalimbali ,”alisema Chacha.
Mbali na hayo naye Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo Bw.Freeman Mbowe alisema idadi ya wapiga kura tu inaonyesha wazi kuwa
ushindi wa kiti hicho cha meya ni lazima uchukuliwe na CHADEMA sababu madiwani wengi wa Mkoa wa Dar es Salaam
wanatoka katika chama hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...