BALOZI wa Uturuki nchini Yesemin Eralp amezindua kampuni mpya ya huduma za tiketi za ndege pamoja na Utalii ya SkyPalm Travel and Tour Ltd.

Tukio hilo lilitokea jumamosi hii hapa jijini ambapo balozi huyo alitoa wito kwa wawekezaji zaidi kujitokeza kuwekeza kwenye sekta hiyo.

Alisema kuwa Tanzania imekuwa ikifanya vema kwenye sekta ya utalii huku ikiwa na vivutio vingi vya utalii vinavyovutia zaidi na kuwavutia watalii kutokea nchi mbalimbali. Aliongeza kuwa wageni kutokea nchi mbalimbali duniani wanahitaji huduma kutokea kwa kampuni bora zaidi itakayowahudumia kwa ufanisi na umakini.

Kwa upande wake Mkuu wa Biashara wa kampuni hiyo Meysun Buyuksarac alisema kuwa kampuni hiyo imelenga kuimarisha utoaji bora wa huduma za usafiri wa ndege pamoja na utalii nchini.

Alisema kuwa Tanzania inazo fursa nyingi za utalii ambapo zimekuwa zikipelekea wageni wengi kujitokeza kuja nchini kutalii, na hivyo kupekekea wageni kutokea nje ya kuja kwa wingi na wao kama kampuni wamejipanga kutoa huduma bora zaidi ili kukidhi uhitaji.
sky palms launch-153
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Yesemin Eralp akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi kampuni mpya ya huduma za tiketi za ndege pamoja na Utalii ya SkyPalm Travel and Tour Ltd.
sky palms launch-146
Mkuu wa Biashara wa kampuni mpya ya huduma za tiketi za ndege pamoja na Utalii ya SkyPalm Travel and Tour Ltd, Meysun Buyuksarac akizungumza katika hafla hiyo.
sky palms launch-51
sky palms launch-147
Baadhi ya Wageni waalikwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...