Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Seka na wafanyakazi wa mgodi wa dhahabu wa MMG Gold Mine Ltd mara baada ya kuwasili mgodini hapo
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya dhahabu ya MMG Gold Mine Ltd, Harrison Abraham (kulia).
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akikagua mgodi wa dhahabu wa MMG Gold Mine Ltd. Kushoto ni Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Harrison Abraham (kulia).
Baadhi ya mitambo ya kuchenjulia dhahabu iliyopo katika mgodi huo wa MMG Gold Mine Ltd uliopo katika kijiji cha Seka, wilaya ya Musoma.
Serikali imetoa miezi minne kwa mgodi wa dhahabu wa MMG Gold Ltd uliopo katika kijiji cha Seka wilaya ya Musoma kuanza uzalishaji vinginevyo itafutiwa leseni.
Agizo hilo limetolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipofanya ziara mgodini hapo kwa lengo la kujionea shughuli zinazoendelea katika mgodi huo.
Awali Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Ziwa Viktoria Mashariki, Mhandisi Juma Sementa alisema leseni ya mwanzo kutolewa kwa mgodi huo ilikua mwaka 2002 ambapo Kampuni ya awali ilikuwa JMG Exploration Co. Limited ambayo ilifanya utafutaji wa madini kuanzia mwaka 2002 hadi 2005.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...