Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inapenda kuujulisha umma kuwa kivuko cha MV Kilombero II ambacho kilizama tarehe 27 Januari 2016, na kusababisha kusimama kwa hudum ya kivuko kwenye Mto Kilombero Mkoani Morogoro kimeanza kufanyakazi rasmi tarehe 29 Februari, 2016 mara baada ya kukamilika kwa ukarabati wake.

Kivuko hicho kinaendelea na ratiba yake ya utoaji huduma ya kivuko kuanzia saa 12:30 asubuhi hadi saa 1:00 jioni kama kawaida. Wizara inaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza wakati kivuko hicho kikiwa kwenye matengenezo.

Taarifa hii imetolewa na,
Eng. Joseph M. Nyamhanga
KATIBU MKUU (UJENZI),
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,
02 Machi, 2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hii picha ya gari iliyokuwa kwenye kivuko mbona inatishia usalama wa raia? Sidhani kama hayo magogo yamefungwa sawasawa,wala sioni kama dereva ameangalia usalama wa haya magogo na usalama wa binadamu.
    Tunaomba madereva na wadau wengine kuangalia suala la usalama kwanza ili kuepuka ajali.
    Ni maoni yangu na mtazamo wangu tu...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...