Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge akielekeza jambo kuhusu wavu uliowekwa kwa ajili ya kuzuia mashabiki wasirukie na kuharibu miundombinu katika maeneo ya vyoo vya uwanja wa Uhuru jana wakati wa kikao cha ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo.
Msanifu wa Majengo na mbunifu wa Mchoro wa Uwanja wa Taifa Aloyce Peter Mushi akifafanua jambo wakati wa kikao cha ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi Bibi. Cecilia Kasongo, Mhandisi wa Uwanja wa Taifa Yusuf, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge, Muhandisi wa mradi wa ujenzi wa uwanja wa Uhuru E. Mwamakunga na Meneja wa Uwanja wa Taifa Rish Urio.
Meneja wa Ujenzi wa Kampuni ya BCEG inayojenga uwanja wa Uhuru Zhang Jiawei akifafanua jambo wakati wa kikao cha ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge, Meneja wa Uwanja wa Taifa Rish Urio, Msanifu wa Majengo na mbunifu wa Mchoro wa Uwanja wa Taifa Aloyce Peter Mushi Muhandisi wa mradi wa ujenzi wa uwanja wa Uhuru E. Mwamakunga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...