Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu akiwa katika Mkutano wa 60 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake ( CSW). Kushoto kwake ni Mwakilishi wa Tanzania wa Kudumu Katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manong.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally
Mwalimu ( Mb) ametoa hutuba kwa niaba ya Kundi la Nchi za Afrika wakati
wa ufunguzi wa Mkutano wa 60 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu
Hali ya Wanawake ( CSW). Mkutano huu wa wiki mbili .
unawakusanya
wawakilishi kutoka serikali mbalimbali duniani na Asasi za Kiraia
ambapo hujadiliana na kubalishana uzoefu na kuelimishana kuhusu hatua
mbalimbali ambazo serikali zao zinachukua katika kuboresha maisha ya
mwanamke na mtoto wa kike.
Wakati
mamia ya wanawake kutoka serikalini na Asasi za Kiraia wakiwa
wanakutana hapa Umoja wa Mataifa kwa mkutano wao unaojadili hali yao
katika maeneo mbalimbali. Mamia mengine ya wanawake hususani wale wa
Afrika wanaendelea kukumbana na changamoto lukuki zinazowarudisha nyuma
kimaendeleo.
Ni
wanawake hao wanaoishi katika nchi zenye migogoro, vita visivyokwisha,
wenye kukabiliwa na uhaba na ukosefu mkubwa wa chakula, maji safi na
salama, matatizo yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi, ndio ambao
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy
Ally Mwalimu(Mb) ameitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza kasi ya
ushirikiano ili malengo mapya ya maendeleo endelevu (Agenda 2030)
yaweze kuwafikia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...