Na Zuena Msuya

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo amepokea ripoti maalumu ya kumaliza mgogoro wa wananchi wa Nyamongo na mgodi wa wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia North Mara uliodumu kwa miaka 6 sasa.

Akizungumza mjini Tarime Mkoani Mara baada ya kupokea ripoti hiyo Prof. Muhongo ameshauri wananchi wa Tarime kuwa watulivu wakati akiendelea kuisoma ripoti hiyo na kutolea majibu mambo yalioyo andikwa katika riporti hiyo.

Profesa Muhongo alisema anaimani mambo yote yalioandikwa katika ripoti hiyo ni mawazo ya wananchi waliohojiwa na  atashangaa endapo kuna mtu atajitokeza  kuikataa.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya Tarime,Glorious Luoga alisema ripoti hiyo itatoa majibu stahiki kwa wanaohitaji kulipwa na hata wasiostahili hivyo wananchi wakae tayari kupokea utekelezaji wa ripoti baada ya kusoma na kupitishwa na Waziri.

Naye Mbunge wa Tarime vijijini John Heche alisema kuwa anaimani na ripoti hiyo kuwa itatenda haki kwa wananchi wake wa Nyamongo ili kutimiza  ahadi ya Rais aliyoitoa wakati akiomba kura kuwa hatamaliza kabisa tatizo la Nyamongo lililodumu kwa muda mrefu.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhandisi John Nayopa alisema kamati hiyo imepokea malalamiko zaidi ya 4400 ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi,malalamiko ambayo yalilenga masuala ya fidia ya ardhi,athari za shughuli za mgodi hasa upande wa mazingira,uvamizi wa mgodi,sakata la tegesha na Askari kutuhumiwa na kunyanyasa na kutesa wananchi.

Kamati hiyo iliundwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo mwezi mmoja uliopita ina wajumbe 27,19 wataaalamu wa Serikali, na Wenyeviti wa vitongoji 80.
Mwenyeki wa kamati John Nayopa akimkabidhi Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo,Taarifa ya kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Nyamongo na Kampuni ya mgodi wa dhahabu ya Acacia North Mara.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo,akionesha taarifa aliyokabidhiwa na Kamati hiyo ambapo ameahidi kuisoma na kuitolea majibu yanayostahili ndani ya kipindi cha wiki tatu tangu Machi 23,2016 alipokabidhiwa taarifa hiyo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, akizungumza jambo mara baada ya kupokea Taarifa ya utekelezaji kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...