Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule, ametembelewa na Viongozi wa ujumbe kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi cha Dar es Salaam, ambao uko nchini Kenya kwa ziara ya mafunzo ya wiki moja. Ujumbe huo unaongozwa na Kamanda wa Chuo cha Ulinzi, Meja Jenerali Yacoub Mohamed, na unajumuisha Maafisa na Washiriki wa Kozi 12.
Makundi mengine matatu kutoka chuo hicho kilichoko Kunduchi yako kwenye ziara kama hii nchini Afrika Kusini, Botswana na Namibia.
 Balozi Haule (kulia) katika mazungumzo na Vingozi waliomtembelea. Wapili kulia ni Meja Jenerali Mohamed na Kushoto ni Mwambata wa Kijeshi Ubalozini, Luteni Kanali Fabian Machemba.
 Meja Jenerali Mohamed akimkabidhi Balozi Jarida lililochapishwa na Chuo cha Ulinzi kwa heshima ya Rais Mstaafu, Mhe. Jakaya Kikwete.
Picha ya Pamoja, Luteni Kanali Maulid Surumbu, Bw. Johnson Nyingi, Mwakilishi wa Jeshi la Kenya, Kanali Sebestian Likaunye, Meja Jenerali Mohamed, Balozi Haule, Luteni Kanali Machemba na Kamishina Msaidizi wa Magereza Phaustine Kasike.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...