Mamia ya waombolezaji, wengi wao wakiwa wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, leo wamejitokeza kuuaga mwili wa mama mzazi wa Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Bw. Absalom Kibanda, leo  asubuhi  huko Masaki jijini Dar es Salaam.
Mama yake mzazi Kibanda, alifariki juzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambako alikuwa akitibiwa ugonjwa wa kiharusi. Mwili wa marehemu Marehemu Mama Gwaseko Kapyela (76)  baada ya kuagwa u mesafiriskwa kwa ndege kuelekea Tukuyu, wilayani Rungwe,  mkoani Mbeya kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi.
Waombolezaji wakimpa pole Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda, na kaka yake wakati wa kuaga mwili wa mama yao mzazi marehemu Marehemu Gwaseko Kapyela Masaki jijini Dar es salaam 
Waombolezaji wakimpa pole Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda, na kaka yake wakati wa kuaga mwili wa mama yao mzazi marehemu Marehemu Gwaseko Kapyela Masaki jijini Dar es salaam 
 Wanahabari nguli Neville Meena na Peter Nyanje wakiandaa shada la maua na msalaba kabla ya safari ya kwenda Tukuyu kuanza
 Safari ikianza
Waombolezaji wakipeleka jeneza lenye mwili wa mama mzazi wa  Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda, baad ya hafla ya  kuaga mwili wa mama yao mzazi marehemu Marehemu Gwaseko Kapyela Masaki jijini Dar es salaam. Kwa picha zaidi ya hafla hii BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...