Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akisalimiana na Viongozi mbalimbali kwenye Ofisi za Mkuu wa Mkoa leo
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye leo tarehe 14 April, 2016 akiwa mkoani Kagera ahaidi kuihamishia Wizara yake kwenye mikoa na Halmashauri za Wilaya kwa wadau wanaohusika ili kurasmisha shughuli na majukumu ya wizara hiyo ili iweze kupata ufanisi. 

Akiongea na wadau mbalimbali wanaohusika na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alisema kuwa lengo la ziara yake ni kuja mikoani kujionea changamoto mbalimbali za wizara yake ili aweze kuzifanyia kazi kwa kuishusha wizara kwa wadau wanaohusika ili kutekeleza majukumu yake. 

Katika kikao hicho Waziri Nape alisema kuwa sekta nne ambazo ni Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zimekuwa hazifanyi kazi zake vizuri kutokana na watendaji wake kutokuwa na idara au vitengo vinavyohusika moja kwa moja na kazi zao jambao ambalo linawafanya kujishikiza katika sehemu au idara nyingine.
Waziri Nape akisaini kitabu kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Picha na Faustine Ruta, Bukoba
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Jackson Msome(kushoto) ambaye alikaimu nafasi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera leo akitoa neno.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...