Wizara ya Nishati na
Madini (MEM) kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania
(TAMIDA), wanawaalika wadau wote wa Sekta ya Madini na wamiliki wa Leseni ya Biashara
za Madini, Masonara na Wachimbaji wa Madini ya Vito kushiriki kwenye Maonesho
ya Tano ya Kimataifa ya Madini ya Vito Arusha (Arusha Gem Fair - AGF).
Maonesho haya yatafanyika katika Hoteli ya
Mount Meru ya Arusha, kuanzia tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
Maonesho ya AGF kwa
mwaka 2016 yanalenga kuendeleza azma ya kuifanya Arusha kuwa kituo Kikubwa cha
madini ya vito Afrika. Pia, maonesho haya yatawakutanisha washiriki (exhibitors) zaidi ya 100 kutoka nchi za
Afrika Mashariki, Kati na Kusini na wanunuzi wa kimataifa zaidi ya 500 pamoja
na wadau mahiri wa tasnia ya vito. Maonesho pia
yanadhamiria kuendeleza biashara ya madini ya vito katika nchi za Mashariki,
Kati na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Kutokana na hilo, Wizara
ya Nishati na Madini haitatoa vibali vyovyote vya kusafirisha madini ya vito
nje ya nchi kuanzia tarehe 5 hadi 28 Aprili, 2016. Ili kuhakikisha kuwa
kunakuwepo na madini ya vito ya kutosha kwenye maonesho haya.
Vibali vitatolewa kwa
Washiriki wa maonesho pekee kuanzia tarehe 19 Aprili, 2016 hadi maonesho
yatakapokwisha. Lengo letu ni kuhakikisha maonesho haya yanafanikiwa na
kuifanya Tanzania kuwa kituo kikubwa cha biashara ya madini ya vito barani
Africa.
Mabanda ya maonesho
yanapatikana kwa gharama za Dola za Marekani 1,000. Kamati ya Maonesho
inasimamia ugawaji wa mabanda hayo kwa ushindani (first come-first be served).
Taarifa kuhusu
usajili zinapatikana katika Ofisi za Madini za Kanda zilizo katika Miji ya
Arusha, Mwanza, Dar es salaam, Mtwara, Mpanda, Shinyanga, Mbeya, Musoma, Songea
na Singida au Ofisi za TAMIDA.
Wanunuzi wanatakiwa kujisajili
kupitia tovuti ya
maonesho: www.arushagemshow.com;
au kwa barua pepe ya maonesho:
info@arushagemshow.com ;
au kwa njia ya simu zifuatazo +255 784352299 or +225 767106773.
Imetolewa
na,
Katibu
Mkuu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...