Wafanyakazi wa NMB wakiwa kwenye picha ya pamoja na wahitimu 30 wa vyuo vikuu ambao wamepata nafasi ya kujifunza kazi za benki katika idara mbali mbali ndani ya benki kwa muda wa miaka miwili na baadae kupata ajira ya kudumu
 Mkurungezi Mtendaji wa NMB- Bi Ineke Bussemaker akiwakaribisha wahitimu 30 wa vyuo vikuu vilivyo ndani nan je ya nchi. Wahitimu hao watapatiwa mafunzo kwa kipindi cha miaka miwili kisha wataajiriwa na Benki katika vitengo mbalimbali vilivyopo makao makuu na kwenye mtandao wa matawi yake ambayo yamesambaa nchini kote.
 Wahitimu 30 wa vyuo vikuu wakimsikiliza kwa umakini Mkurungezi Mtendaji wa NMB Bi Ineke Bussemaker 


  • Ni waliosomea nchini na nje ya nchi
  • Kupatiwa mafunzo maalumu ya ndani ya kazi kwa kipindi cha miaka miwili

NMB imeajiri wahitimu 30 waliosoma vyuo vikuu nchini na nje ya nchi katika mpango wake wakukuza vipaji kwa wahitimu wa vyuo vikuu ulioanzishwa mwaka jana. Wahitimu hao watapatiwa mafunzo ya ndani kwa kipindi cha miaka 2 kisha wataajiriwa na Benki katika vitengo mbalimbali vilivyopo Makao makuu na kwenye mtandao wa matawi yake ambayo yamesambaa nchini kote.

Mkakati mmojawapo wa NMB, ni kuunga mkono jitihada za serikali kukuza uchumi ikiwa ni pamoja na kuongeza fursa za ajira nchini hususani kwa vijana wanaohitimu masomo ya vyuo vikuu. Awamu hii ni ya pili ya mpango huu wakuwapatia mafunzo ya kazi ya miaka 2 wahitimu wa vyuo vikuu waliofanya vizuri katika fani walizokuwa wanasomea kisha kuwapatia ajira.

Katika mchakato wakuwapata wahitimu hawa kulikuwepo na waombaji wapatao 312 ambapo baada ya jopo la wataalamu kupitia maombi hayo kwa umakini liliweza kutoa majina ya wahitimu 125 ambao walifanyiwa usahili na tathmini katika maeneo mbalimbali. Zoezi hili lilifanyika kwa uwazi na umakini mkubwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa kwa wenye sifa za kuingia kwenye mpango huu kama ambavyo ilitangazwa kabla ya kuanza zoezi la kupata waombaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa NMB – Bi Ineke Bussemaker amesema kuwa NMB ni moja ya mwajiri mkubwa katika sekta ya benki nchini ikiwa imeajiri wafanya kazi zaidi ya 3,000 na ikiwa inawajali wafanyakazi wake wa kuwajengea mazingira mazuri ya kazi.

Akiongea na waandishi wa habari, Bi Ineke Bussemaker alisema, “Nafurahi kuwa benki yetu imekuwa kipaumbele kuwaajiri vijana hawa ambao watapatiwa mafunzo mbalimbali kuhusiana na sekta ya kibenki katika ofisi zetu za makao makuu na kwenye matawi yetu zaidi ya 175 ambayo yamesambaa nchi nzima. Muhimu zaidi nina furaha kuwa kwenye uchaguzi wa zoezi hili, tumechagua wanawake 15 na wanaume 15 bora katika kundi hili.”

Katika kipindi cha miaka 10 tangu NMB ibinafsishwe mnamo mwaka 2005 imeongeza ajira zaidi ya 1,500 ambapo kwa sasa inao wafanyakazi wapatao 3,140. Benki inajivunia kujenga mazingira bora kwa wafanyakazi wake kwa kufuata misingi ya ajira inayokubalika kitaalamu na mwaka hadi mwaka imekuwa ikiboresha hali inayoifanya kuwa sehemu nzuri inayovutia wengi kutaka kuwa waajiriwa wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hatua ya kuwezesha wahitimu wetu wa vyuo vikuu ni nzuri ya kuigwa na waajiri wengine. Hawa vijana ukiwawezesha kuelewa kazi unaweza kukaa nao kwa muda mrefu tuwezeshe wahitimu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...