Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) yatoa mkopo wa 890 Milioni kwa wakulima wa zao la mpunga wanaojishughulisha kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mkula wilayani Kilombero ili kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga.
Hayo yaliwekwa bayana na Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal wakati wa warsha ya wakulima wadogo zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Bw. Paschal alisema lengo la mkopo huo unaowanufaisha zaidi ya wakulima 350 ni kuongeza tija na uzalishaji wa mpunga ili Kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania na kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.
“Mkopo huu na mengine tunayotoa imelenga kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo ili kusaidia kukabiliana na mapungufu hayo na kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi katika kilimo nchini,” alisema Bw. Paschal.
Mkurugenzi
wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal (aliyesimama)
akiwasilimia wakulima wadogo zaidi ya 340 (hawapo pichani) wa mkoa wa
Morogoro wakati warsha ya wakulima wadogo zaidi ya 340 wa Mkoa wa
morogoro iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya
ya Kilombero. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Lephy Gembe.
Mkuu
wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Lephy Gembe (aliyesimama) akiwasilimia
wakulima wadogo zaidi ya 340 (hawapo pichani) wa mkoa wa Morogoro wakati
warsha ya wakulima wadogo zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro iliyofanyika
katika Ukumbi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero. Kushoto
Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal.
Mkurugenzi
wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal (Kulia) akiwasilisha
Mada ya Utambulisho wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo kuhusu Huduma
zitolewazo na Benki, Mpango shirikishi wa Kumsaidia Mkulima Mdogo kupata
mkopo na utalaam wa kilimo cha kisasa kwa kuwashirikisha wadau wakuu wa
Kilimo katika kumkwamua mkulima mdogo wakati warsha ya wakulima wadogo
zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira
Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Mkuu
wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Lephy Gembe (Wapili kushoto) akizungumza
na Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal (Wapili
kulia) wakati warsha ya wakulima wadogo zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro
iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya
Kilombero.
Mkuu
wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Lephy Gembe akiwa katika picha ya pamoja
na baadhi ya wakulima wadogo waliohudhuria warsha ya wakulima wadogo
zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira
Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...