KAMPUNI ya Dar Brew, imezindua chupa mpya ya bia ya asili ya Chibuku Super yenye ujazo wa mililita 750, ambayo mtumiaji halazimiki kurudisha chupa pale anapoitumia.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo, Meneja Masoko wa Dar Brew, Oscar Shelukindo alisema, bia hiyo iliyopo katika chupa nzuri ya plastiki inayovutia, itauzwa kwa bei ya Sh 1,000 tu kwa kila chupa.
“Bia hii imetengenezwa kwa utaalam wa hali ya juu na kwa kutumia mitambo ya kisasa kabisa, hivyo tunawahakikishia watumiaji ubora wa hali ya juu,” alisema.

Shelukindo alisema, bia hiyo imetengenezwa kwa kutumia malighafi za hapa nyumbani, ikiwemo nafaka ya mtama ulio bora, hivyo kuna kila  sababu kwa Watanzania kujivunia kilicho chao na kukumbuka asili yao, kwani hii ni bia yao ya asili.

Naye Meneja Mauzo na Usambazaji wa Dar Brew, Fred Kazindogo alisema, bia hiyo itaanza kupatikana nchi nzima katika baa, maduka makubwa (Super Markets), katika maduka ya jumla na rejareja na sehemu zinazouzwa vileo kuanzia leo.

Kazindogo alisema, ana imani kubwa wapenzi wa bia wataipokea kwa shangwe na wataitumia ili kuonesha wanajali asili yao.
Meneja Masoko wa Dar Brew, Oscar Shelukindo akizungumza wakati wa kuzindua chupa mpya ya bia ya asili ya Chibuku Super yenye ujazo wa mililita 750, jijini Dar es salaam leo. Kulia ni Meneja Mauzo na Usambazaji wa Dar Brew, Fred Kazindogo.
Meneja Mauzo na Usambazaji wa Dar Brew, Fred Kazindogo akifafanua jambo juu ya ujazo wa chupa hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...