Marehemu Askofu mstaafu Christopher Ruhuza
02/02/1922 - 06/03/2016
Familia ya Marehemu Askofu Mstaafu Christopher Gwassa RUHUZA wa Dayosisi ya Kanisa Anglikana Kagera, Ngara, inapenda kukualika kushirikiana nayo kwenye misa Maalum ya kumaliza msiba wa Baba/Babu yao CHRISTOPHER RUHUZA aliyefariki tarehe 06/03/2016 na kuzikwa tarehe 11/03/2016 Kanisa Kuu Anglikana Murugwanza Ngara.
Misa hiyo kwa Dar es Salaam itafanyika Kanisa Anglikana St Albans iliyopo maeneo ya Posta mpya katikati ya Mji.
Misa itafanyika Jumamosi, tarehe 14/05/2016, saa tatu na nusu asubuhi.
Ushiriki wako kwenye misa ni faraja kubwa sana kwetu.
Mungu akubariki sana.
Zaburi 23.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...