Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO


Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wamekanusha kudaiwa fidia na wananchi wa Kijiji cha Mazingira,Wilaya ya Handeni mkoani Tanga waliovunjiwa nyumba zao ili kupisha ujenzi wa barabara.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Meneja wa TANROADS Mhandisi Alfred Ndumbaro alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hii juu ya malalamiko ya wananchi wa Kijiji hicho kuhusu kutolipwa fidia zao.

”Sheria iko wazi kuwa wanaojenga karibu na barabara wakivunjiwa hawalipwi fidia yoyote lakini wale ambao ujenzi wa barabara uliwafuata katika maeneo yao wana haki ya kulipwa fidia”, alisema Mhandisi Ndumbaro.

Mhandisi Ndumbaro ameongeza kuwa zoezi la malipo ya fidia kwa wanakijiji waliokuwa na uhalali wa malipo hayo lilishakwisha zamani kwa hiyo, wanaodai sasa ni wale ambao nyumba zao zilivunjwa kutokana na kujenga eneo la barabara.

Aidha, Mhandisi huyo ametoa rai kwa wananchi kufuata sheria za ardhi ili kupata uhalali wa viwanja vyao pamoja na kuepuka usumbufu na gharama za kuvunjiwa nyumba zao.

Nyumba hizo zilivunjwa ili kupisha ujenzi wa barabara ya lami yenye Kilomita 54 kutoka Mkata hadi Handeni iliyojengwa na Kampuni ya Synohydro Corporation Limited ya China.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...