Wakati Coastal Union ya Tanga ikiwa imeaga rasmi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania 2015/16, swali linabaki kwa wadau wa soka nchini kwamba ni timu gani itaungana na Wagosi wa Kaya kushuka daraja kutokana na timu tano kuwa katika hatari?
Pazia la msimu wa Ligi Kuu 2015/16 linatarajiwa kufungwa Jumapili ijayo Mei 22, mwaka huu na timu tano zinazoonekana kuwa katika hatari ya kuungana na Coastal Union yenye pointi 22 (nafasi ya 16) kushuka daraja. Kati ya timu hizo tamo, mbili ndizo zitaungana na Coastal kushuka daraja hivyo kuwa na jumla ya timu tatu.
Kwa taarifa zaidi fuata link hapo chini



SERENGETI BOYS ANA KWA ANA NA INDIA
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 maarufu kama Serengeti Boys, Bakari Shime amesema hana wasiwasi kuwavaa India-wenyeji wa michuano maalumu ya soka ya kimataifa kwa vijana (AIFF Youth Cup 2016 U-16) yaliyoandaliwa na Shirikisho la Soka nchini humo (AIFF).
Shime ambaye kikosi chake kilitoka sare ya 1-1 na Marekani Jumapili ya Mei 15, 2016, kesho Jumanne kikosi chake kitawavaa India kwenye Uwanja wa Tilak Maidan, Vasco jijini Goa kabla ya kuahidi kuwatungua wenyeji hao kwenye michuano hiyo inayofanyika ikiwa ni kuipa baraka India kabla ya fainali za kombe la Dunia kwa vijana mwakani-2017.

Kwa taarifa zaidi fuata link hapo chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...