Uelewa mdogo kuhusiana na sumu aina ya aflatoxin hapa Tanzania umesababisha vita dhidi yake kuwa na changamoto.
Aflatoxins ni kemikali yenye sumu inayoweza kusababisha saratani; huzalishwa na aina ya fangasi wanaoishi katika udongo au mimea na nafaka zinazooza.Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Florens Turuka amesema hali hiyo inasababisha usalama mdogo wa chakula na kuhatarisha afya za walaji.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo, hali hiyo sio tu inahatarisha afya za walaji, bali pia kuharibu biashara ya bidhaa za mazao hasa nafaka.Alikuwa akiongea wakati wa mkutano uliozungumzia mapambano dhidi ya sumu hiyo hapa nchini. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Pamoja na mambo mengine, wajumbe wa mkutano huo walijadili namna bora ya kuhusisha mapambano ya sumu hiyo kwenye miradi, programu na mipango mbalimbali.Kwa sababu hiyo, Dkt. Turuka alisema, serikali itatoa kila aina ya ushirikiano kuhakikisha kuwa juhudi zote za mapambano dhidi ya aflatoxin zinafanikiwa.“Serikali itafanyia kazi mapendekezo ya mkutano huu ili kupata mafanikio,” alisema.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo, aflatoxin ni tatizo kubwa kwenye mfumo wa chakula hapa nchini hasa mahindi, karanga na maziwa.Vyakula hivi ni kati ya vinavyoliwa kwa wingi hapa nchini.Dkt. Turuka alisema bado juhudi kubwa zinatakiwa kufanywa ili kuondokana na tatizo hilo ambalo huweza kusababisha saratani ya ini.
Utafiti wa hivi karibuni umeonyesha kuwa maeneo ya ukanda wa Mashariki na Magharibi hapa nchini ndio yaliyoathirika zaidi na sumu hiyo katika mfumo wa vyakula.Aliishukuru Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa juhudi zake za kudhibiti aflatoxin na timu nzima ya Partnership for Aflatoxin Control in Africa (PACA) kwa kuratibu mkutano huo.
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na wajumbe kutoka nchi za Gambia, Malawi, Senegal na Uganda.PACA inafanya kazi na serikali za Afrika katika kupambana na kudhibiti changamoto ya aflatoxin.
Aflatoxins ni kemikali yenye sumu inayoweza kusababisha saratani; huzalishwa na aina ya fangasi wanaoishi katika udongo au mimea na nafaka zinazooza.Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Florens Turuka amesema hali hiyo inasababisha usalama mdogo wa chakula na kuhatarisha afya za walaji.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo, hali hiyo sio tu inahatarisha afya za walaji, bali pia kuharibu biashara ya bidhaa za mazao hasa nafaka.Alikuwa akiongea wakati wa mkutano uliozungumzia mapambano dhidi ya sumu hiyo hapa nchini. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Pamoja na mambo mengine, wajumbe wa mkutano huo walijadili namna bora ya kuhusisha mapambano ya sumu hiyo kwenye miradi, programu na mipango mbalimbali.Kwa sababu hiyo, Dkt. Turuka alisema, serikali itatoa kila aina ya ushirikiano kuhakikisha kuwa juhudi zote za mapambano dhidi ya aflatoxin zinafanikiwa.“Serikali itafanyia kazi mapendekezo ya mkutano huu ili kupata mafanikio,” alisema.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo, aflatoxin ni tatizo kubwa kwenye mfumo wa chakula hapa nchini hasa mahindi, karanga na maziwa.Vyakula hivi ni kati ya vinavyoliwa kwa wingi hapa nchini.Dkt. Turuka alisema bado juhudi kubwa zinatakiwa kufanywa ili kuondokana na tatizo hilo ambalo huweza kusababisha saratani ya ini.
Utafiti wa hivi karibuni umeonyesha kuwa maeneo ya ukanda wa Mashariki na Magharibi hapa nchini ndio yaliyoathirika zaidi na sumu hiyo katika mfumo wa vyakula.Aliishukuru Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa juhudi zake za kudhibiti aflatoxin na timu nzima ya Partnership for Aflatoxin Control in Africa (PACA) kwa kuratibu mkutano huo.
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na wajumbe kutoka nchi za Gambia, Malawi, Senegal na Uganda.PACA inafanya kazi na serikali za Afrika katika kupambana na kudhibiti changamoto ya aflatoxin.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...