Na Daudi Manongi-MAELEZO
UONGOZI Chuo Kikuu cha Dar es salam unatarajia kununua taa
za dharura 12 kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la giza katika
Hosteli ya Mabibo.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Naibu Makamu
mkuu wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anaeshughulikia
masuala ya Utawala Prof.David Alfred Mfinanga wakati wa
mahojiano na Idara ya Habari.
Alisema kuwa tatizo la giza nene katika eneo hilo la lango kuu la
kuingia Hostel za mabibo mpaka eneo lile la maegesho ya magari
lipo mbioni kupatiwa ufumbuzi baada ya taratibu za ununuzi
kukamilika.
Alisema kuwa kukamilika kwa uwekaji wa taa hizo za dharura
zitapunguza kabisa tatizo hilo.
Aidha, Prof.David Alfred Mfinanga alisema kuwa katika mpango
wa muda mrefu wa kutatua tatizo hizo uongozi wa UDSM
unatarajia kuweka umeme wa jua ambao utapunguza gharama
za kulipia umeme na hivyo kuwa na umeme wa uhakika.
Hostel hizo za kisasa zilizojengwa miaka michache iliyopita na
Shirika la Hifadhi za Jamii(NSSF) zimesaidia kupunguza tatizo la
makazi lililopo kampasi kuu ya Chuo kikuu(mlimani) lakini
kasoro hizi za kukosa umeme zinahatarisha eneo hilo kugeuka
kuwa la ubakaji na hata ukabaji kwa wanafunzi na wageni.
taa hizo ni mkandarasi ndiyo aliyesahau ni wajibu wake. hizo pesa zifanye kazi nyingine
ReplyDelete