Teknolojia imeendelea kurahisisha maisha na kwa sasa kumekua na ukuaji wa matumizi ya simu za viganjani kufanya miamala ya fedha maeneo mengi ya bara la Afrika. Kufuatia ongezeko kubwa la watumiaji wa simu, mabenki na kampuni za simu zimeendelea kuhakiki simu zinatumika kufanya miamala ya kifedha.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka jana (2015) ya GSMA State of the industry, huduma za kifedha kupitia simu kwa sasa zinapatikana katika nchi 93 duniani ikiwa na jumla ya huduma 271 kwa ujumla wake, kwa wastani watoa huduma za kifedha kupitia simu wana safirisha kiasi cha dola milioni 33 kwa siku. Takwimu hizi  zinategemewa kuendelea kukua.

Aidha, Mwaka jana (2015), European investment bank ilianisha Afrika kuongoza duniani kwa matumizi ya Simu za viganjani kufanya miamala yakifedha. Kwa Upande wa Nchi ya Kenya, asilimia 62 (62%) ya watu wake wamekua wakitumia simu za viganjani kufanya miamala ya kifedha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...