Bank ABC imeanzisha huduma mpya kwa wafanyabishara wakubwa kuhamisha and kuingiza mitaji yao ndani na nje ya nchi kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya elektroniki.Akizungumza katika hafla iliyofanyika Jumatano hii, Mkuu wa kundi la Benki hiyo katika ukanda wa Afrika, Dk. Mabouba Diagne alisema wametenga Dola za Kimarekani milioni 20 (zaidi ya Sh billion 40) kwa ajili ya mpango huo unaolenga kuimarisha biashara miungoni mwa nchi za Afrika.
“Tumeanzisha huduma hii mpya kwa ajili ya kurahisisha na kukuza biashara miungoni mwa wafanyabishara wakubwa barani Afrika. Tunataka wafanyabiashara waweze kufungua milango yenye fursa nyingi za kibishara barani Afrika,” Dk. Diagne alisema.Alisema Banc ABC imezimia kuwawezesha Watanzania kutumia teknolojia mpya ya kuhamisha mitaji na fedha nyingi si ndani ya nchi tu bali nje ambako kuna fursa nyingi za biashara zisizotumika.
“Mara nyingi wafanyabishara wengi wa hapa nchini wanaofanyabishara nan chi jirani wamekuwa wakilalamika kukosekana kwa huduma bora za kuhamisha fedha kwa wingi. Sasa jawabu limepatikana kwa Banc ABC kuanzisha huduma za kisasa za kuhamisha mitaji,” alisema.
Alisema watu wanaweza kuhamisha mitaji hata fedha nyingi nchi za nje kwa kutumia simu za mkononi bila kuathiri biashara.“Tumeanzisha huduma hii kwa sababu biashara baina ya nchi za Afrika ni jambo muhimu la kuwezesha nchi na wafanyabishara waweze kutumia fursa nyingi zilizomo barani Afrika kutokana na bara hili kuwa na rasilimali nyingi asilia,” alisema kiongozi huyo msomi mwenye shahada ya juu ya uzamili ya hisabati.
Alisema suala la kubadilishana na kuhamisha mitaji ni biashara kubwa duniani kwa sababu mitaji ni bidhaa muhimu kwa maendeleo ya nchi na watu.Mapema mkurugenzi wa Banc ABC Tanzania, Bw Dana Botha alisema tayari benki hiyo imeanzisha mtandao wa matawi 100 hapa nchini na kuwa miungoni mwa benki imara.Naye Mtendaji Mkuu wa kundi la benki hiyo Dk. Blessings Mudavanhu alisema kuwa benki hiyo ambayo imesajiliwa katika soko la fedha la London, ilizindua aina ya bidhaa yake mpya na kujitanua kimataifa baada ya kuungana na Atlas Mara.
“Tutatumia jamvia la teknolojia ya habari na mawasiliano. Tunataka watu waanchane na kuandika cheki nyingi na kutumia gharama kubwa za miamala ya katatazi badala yake watumie simu za mkononi,” alisema Dk Madavanhu.Alisema benki hiyo ambayo inaendesha biashara katika nchi za Tanzania, Nigeria, Afrika kusini, Botswana Zimbabwe, Rwanda, Burundi na Zambia imedhamiria kuwa benk kubwa inayokuza biashara miungoni mwa nchi za Afrika.
Mkurugenzi
Mtendaji wa BancABC Tanzania Bwana. Dana Botha (wa pili kulia),
akibadilishana mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla
waliyowaandalia wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika
kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara.
Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wanaomsikiliza kutoka
kushoto ni, John Kazimoto, Jones Mwalemba, naJohn Du Toit.
Mkuu
wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni wa Kundi la BancABC, Dk.
Mabouba Diagne (wa pili kulia), akibadikishana mawazo na baadhi ya
wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia wateja wao
kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma
bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika
jijini Dar es Salaam juzi.
Mkuu
wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni wa Kundi la BancABC, Dk.
Mabouba Diagne (wa pili kulia), akimsikiliza mmoja wa wateja wa benki
hiyo, John Du Toit katika hafla waliyowaandalia wateja wao kuwajulisha
mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki
chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam
juzi.
Mkuu
wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni BancABC Tanzania,
Khalifa Zidadu (kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo
katika hafla waliyowaandalia wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki
hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la
atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto ni
Ofisa Fedha Mkuu wa Superdoll, Sateesh Babu Desu na Prasanthar Govinder
pia wa Superdoll.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...