Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi,Vijana na Ajira, Antony Mavunde (kushoto), akipokea msaada wa madawati 50 yenye thamani ya zaidi ya sh milioni 6 kutoka kwa Mkurungenzi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma, Rehema Hamisi yaliyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya Shule ya Msingi Makole iliyopo Manispaa ya Dodoma,mwishoni mwa wiki

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony Mavunde (wa pili kushoto), akifurahi pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Makole iliypo manispaa ya Dododma mara baada ya makabidhiano ya msaada wa madawati 50 uliotolewa na wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma, wengine katika picha ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Dk. Jasmin Tsekwa (wa pilikulia) na kulia ni Mkurungenzi Benki ya CRDB tawi la Dodoma, Rehema Hamisi. 

Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma wakiwa wamekaa kwenye madawati ambayo waliikabidhi shule ya msingi makole iliyomjini Dodonma jana ,msaada huo unathamani ya zaidi ya sh milioni 6.

Mkurungenzi Benki ya CRDB tawi la Dodoma Rehema Hamisi (kulia) akisalimiana na wanafunzi wa Shule ya Msingi Makole iliyopo mjini Dodoma, baada ya kuwakabidhi msaada wa madawati 50 yaliyotolewa na wafanyakazi wa wa benki hiyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali kupunguza tatizo la madawati mashuleni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...